Luka 18:31-33
Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu,
na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii. Kwa kuwa
atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyanyiwa dhihaka; atatendewa jeuri, na
kutemewa mate; nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.
1 Yohana 1 :1
Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu,
tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno ya uzima.
Matendo 2:14-36
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kmi na mmoja, akapaza sauti yake,
akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo
hili, mkasikilize maneno yangu. Sivyo mnavyodhank; watu hawa hawakuelewa, kwa
maana ni saa tatu ya mchana; lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa
cha nabii Yoeli. Itakuwa siku ya mwisho, asema Mungu, nitamwagia watu wote Roho
yangu, na wana wenu na binti zenu watabiri; na vijana wenu wataona maono; na
wazee wenu wataota ndoto.
Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake. Roho yangu,
nao watatabiri. Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi
chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa
damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri. Na itakuwa
kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu
aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu
alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; mtu huyu
alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani,
ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; ambaye Mungu alimfufua,
akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikiwe nao. Maana Daudi
ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande
wangu wa mkono wa kuume, nisitikisike. Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi
wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini. Kwa maana
hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.
Umenijulisha njia za uzima. Utanijaza furaha kwa uso wako. Waume, ndugu zangu,
mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya
kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. Basi kwa kuwa ni
nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno
vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi. Yeye mwenyewe akitangulia
kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake
haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu. Yesu huyo Mungu alimfufua,
na sisi sote tu mashahidi wake. Basi yeye, akiishi kupandishwa hata mkono wa
kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu
hiki mnachokiona sasa na kukisikia. Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye
mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa
kuume. Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yaho. Basi nyumba yote ya
Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amefanya Yesu huyo mliyemsulubisha kuwa
Bwana na Kristo.
Luka 24 :1-11
Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini,
wakiyaleta manukato waliyoweka tayari. Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa
mbali na kaburi, wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu. Ikawa walipokuwa
wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao,
wamevaa nguo za kumeta-meta; nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata
nchi, hao waliwaambia, kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? Hayupo hapa,
amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya, akisema,
Imempasa Mwana wa Adamu kutiwa mikononi mwa wenye dhambi, na kusulibiwa, na
kufufuka siku ya tatu. Wakayakumbuka maneno yake. Wakaondoka kaburini, wakarudi;
wakawaarifu wale kumi na mmoja na wengine wote habari za mambo hayo yote. Nao ni
Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo, na wale wanawake wengine
waliokuwa pamoja nao; hao waliwaambia mitume habari ya mambo hayo.
Yohana 3:1-8.
Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.
Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa
Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe,
isipokuwa Mungu yu pamoja naye. Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia,
Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
Ufunuo 3:20
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua
mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Mathayo 28:20
na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja
nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Waebrania 13:5
Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye
mwenyewe amesema, Kitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.
Ufunuo 3:20
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua
mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Wakolosai 1:14
Ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi.
Yohana 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale
waliaminio jina lake.
2 Wakorintho 5:14,15,17
Maana, upendo wa Kristo watubidisha; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja
alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote; tena alikufa kwa ajili ya wote
ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili
yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao...Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya
Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
Yohana 15:7
Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo
lote nanyi mtatendewa.
Matendo 17:11
Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea
lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba
maandiko hayo ndivyo yalivyo.
Yohana 14:21
Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye
atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhirisha kwake.
Mathayo 4:19
Akawaambia, Nifaateni, nami nitawafanya kuwa maana walikuwa wavuvi.
Yohana 15:8
Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.
1 Petro 5:7
Huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishugulisha sana kwa
mambo yenu.
Wagalatia 5:16-18
Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa
sababu mwili hutamani ukishindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata
hamwezi kufanya mnayotaka.
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa
mashahidi wangu katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Waebrania 10:25
Wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane;
na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Isaya 53:6
Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe;
Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
Warumi 8:9
Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamfuati mwili; bali
mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
2 Wakorintho 3:18
Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama
vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata
utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana aliye Roho.
Matendo 5:3-5
Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho
Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako,
hakikuwa mali yako? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa
kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuaje hata ukaweka
neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania
aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote
walioyasikia haya.
1Wakorintho 3:16
Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa
ndani yenu?
Yohana 14:26
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,
atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Warumi 8:26
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi
itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
1 Yohana 4:14
Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa
ulimwengu.
Wagalatia 5:22, 23
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili,
uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu;
nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa
nchi.
Warumi 8:9
Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamfuati
mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo,
huyo si wake.
Wagalatia 5:22-23
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili,
uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Matendo Ya Mitume 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu;
nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa
nchi.
Mathayo 5:6
Heri wenye njaa na kiu ya haki; maana hao watashibishwa.
I Yohana 1:9
Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi
zetu na kutusafisha na udhalimu wote.
Waefeso 5:18
Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
1 Yohana 5:14-15
Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi
yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba
tunazo zile haja tulizomwomba.
Wagalatia 5:22-23
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili,
uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Yakobo 5:16
Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
2 Timotheo 3:16
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu
makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaabidisha katika haki;
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu;
nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa
nchi.
I Kor. 10: 13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni
mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile
jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
2 Petro 1:3-11
Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa,
kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake an wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo
ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa
washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu
iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na
katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika utauwa wenu
upendano wa ndugu, upendo. Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele,
yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana
we Yesu Kristo. Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu
vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake zaidi kufanya imara kuitwa
kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe. Maana hivi
mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana wetu, Mwokozi
wetu Yesu Kristo.
Waebrania 11:6
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu
lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
1 Yohana 5:1-5
Kila mtu aaminiye kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu
ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye. Katika hili
twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri
zake. Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri
zake si nzito. Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu;
na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. Mwenye kuushinda
ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?
1 Yohana 4:1-4
Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na
Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Katika hili mwamjua
Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili
yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo
roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako
duniani. Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu
yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.
1 Yohana 5:11-13
Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo
katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu
hana huo uzima. Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa
milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu.
Waebrania 10:25
Wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane;
na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
1 Wakorintho
2:14
Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mamabo ya Roho wa Mungu; maana kwake
huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya
rohoni.
1 Wakorintho 3:1-3
Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya
rohoni, bali kama kama na watu wenye tabia ya mwiline, kama na watoto wachanga
katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa
hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa
tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! si watu wa tabia
ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?
Warumi 7:15, 18, 24
Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo,
silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda...Kwa maana najua ya kuwa
ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka
nataka, bali kutenda lililo jema sipati...Ole wangu, maskini mimi! ni nani
atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
|